
RAIS Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa,
umoja na mshikamano wa Waislamu ndio njia pekee itakayoweza kuwaokoa na
misukosuko mbalimbali.
Akizungumza na kundi la wanasiasa, viongozi wa
kidini na wasomi wa Pakistan mjini Islamabad, Rais Ahmadinejad ameongeza
kuwa kuna ulazima wa kubainishwa kwa uwazi masuala ya kimsingi
ulimwenguni.
Ameongeza kuwa, watu wa Ulaya na Marekani na jamii yote ya
mwanadamu inaishi chini ya ukandamizaji, dhulma na unyanyasaji.
Akielezea njama zinazofanywa na maadui zenye shabaha ya kuleta hitilafu
kati ya watu wote ulimwenguni, Rais wa Iran amesema kuwa, Wazayuni na
Marekani wanafanya njama za kuibua mifarakano kati ya watu wote
ulimwenguni ili waweze kufanikisha malengo na maslahi yao haramu.
Katika
sehemu nyingine ya hotuba yake Rais Ahmadinejad amesema kuwa, Wazayuni
na waitifaki wao na hali kadhalika Marekani wamekuwa dhaifu mno na
kwamba wananchi wa Gaza wameweza kusimama kidete na hatimaye kujipatia
ushindi kwenye vita vya siku nane kati yao na utawala wa Kizayuni wa
Israel.

0 comments:
Post a Comment