BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JARIBIO LA MAPINDUZI YA KIJESHI LAZIMWA NCHINI LIBYA.

 http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/96150a3351646aa118f66bad193da703_XL.jpg
DURU za habari kutoka Libya zinaripoti juu ya kuzimwa jaribio la mapinduzi ya kijeshi yaliyopangwa na  maafisa wa zamani wa jeshi la nchi hiyo. 
Taarifa zinasema kuwa, kundi la kwanza la maafisa hao tayari limeshakamatwa katika mji wa Benghazi mashariki mwa nchi hiyo, huku shirika la kijasusi la kijeshi la Libya likiendelea na msako wa kuwatia mbaroni viongozi wengine wa mtandao huo huko Tripoli. 

Hii ni mara ya kwanza kutokea jaribio la mapinduzi ya kijeshi nchini Libya tokea alipong'olewa madarakani dikteta Kanali Muammar Gaddafi. 

Hivi karibuni kumetokea mauaji yanayofanywa na watu wasiojulikana  dhidi ya viongozi wa kisiasa na kijeshi nchini humo, miongoni mwao wakiwemo AbdulFattah Younnis aliyekuwa Kamanda wa Operesheni za kijeshi dhidi ya vikosi vya Gaddafi katika kipindi cha  vita vilivyotokea mwaka uliopita nchini humo, na Kanali Faraj al Darsi Kamanda wa Usalama wa Benghazi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: