BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SIKIA HII KUTOKA AFRIKA YA KUSINI, AFUNGWA MIAKA 40 KWA PEMBE ZA VIFARU.

 
Vifaru wanakabiliwa na tisho la kuwindwa kiharamu.
 
MAHAKAMA nchini Afrika Kusini imemhukumu kifungo cha miaka arobaini raia mmoja wa Thailand aliyepatikana na hatia ya kuuza pembe za vifaru na kuandaa maonyesho ya uwindaji yasiyokubalika.

Chumlong Lemtongthai alikiri kosa la kuwalipa makahaba kuweza kufanya maonyesho ya uwindaji wa vifaru.

Pembe hizo ziliuzwa barani Asia ambako soko la pembe hizi ni kubwa sana kwani hutumiwa kama dawa.

Zaidi ya vifaru miatano wameuawa nchini humo na wawindaji haramu mwaka huu pekee.

Akitoa hukumu hiyo jaji alisema kuwa hataki wajukuu wake wakuwe bila kujionea vifaru nchii humo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: