BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

ZAIDI YA WATU 7.7 NCHINI NIGERIA WAATHIRIKA NA MAFURIKO.

MASHIRIKA ya Umoja wa Mataifa yamesema mafuriko nchini Nigeria yameathiri zaidi ya watu milioni 7.7. Mafuriko hayo ambayo yameelezewa kuwa mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40, yamesemekana kuwaua zaidi ya watu mia tatu, huku wengine zaidi ya milioni mbili wakiwa wamejiandikisha kama wakimbizi wa ndani.

Shirika la Afya Duniani, WHO limesema visa vya maambukizi ya ugonjwa wa malaria vimeongezeka kutokana na mafuriko hayo, ingawa hakuna mlipuko mkubwa ulioripotiwa. WHO pia imeeleza uharibifu uliofanyika dhidi ya majengo na vifaa vya afya katika maeneo yaloathirika.

Nalo Shirika la Kuhudumia Watoto, UNICEF, limesema maeneo yaloathirika hayana huduma za maji safi, kwani asilimia 63 ya maji ya kunywa na kupikia hutoka kwenye mito na visima vilivyo wazi.

Afisi ya kuratibu misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa, OCHA limesema ingawa mafuriko hayo yanapungua, mashirika ya kibinadamu yanakadiria kuwa gharama ya mahitaji ya kibinadamu ni dola milioni 38, hasa katika majimbo 14 yaliyoathirika zaidi. Jens Laerke ni msemaji wa OCHA.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: