BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

TANZANIA IPO TAYARI KUIPIGA TAFU DRC KUWAONDOA WAASI WA M23.

 
 Watu wakikimbia mapigano ya waasi katika mji  wa Goma nchini Congo mji huo una utajiri mkubwa wa madini.
  
SERIKALI ya Tanzania imesema iko tayari kutoa bataliani moja ya wanajeshi  800 ili waweze kuingilia kati vita vinavyoendelea nchini Kongo kama Umoja wa Mataifa (UN), utatoa kibali cha kuruhusu kufanyika hivyo.

Msimamo huo wa Serikali umetolewa huku juhudi za kutafuta namna ya kutafuta suluhu ya mgogoro huo zikiendelea mjini Kampala, Uganda, ambapo viongozi wa nchi zinazopakana na DRC wakikutana kutafuta msimamo wa pamoja.

Kauli hiyo ya Membe imetolewa wakati wapiganaji wa M23 wanaoipinga Serikali ya Kongo wakisisitiza kwamba sasa hivi wanajipanga kupambana kuelekea Bukavu, Kisangani kisha mji mkuu wa nchi hiyo, Kinshasa.

Pia, imeitaka UN kutoa kibali cha kuyaruhusu majeshi ya umoja huo yanayolinda amani nchini Kongo kupambana waasi hao wa M23 ili kuweza kuwang’oa na kuleta amani Mashariki mwa nchi hiyo.

Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

“Sisi nchi za SADC na maziwa makuu tukiruhusiwa tukienda tuna uwezo wa kupambana na kuwaondoa hao M23 wanaosumbua lakini tunachohitaji ni ruhusa kutoka UN kwani wanajeshi wanaohitajika kufanikisha hilo ni 4,000,” alisema Membe na kuongeza;

“Hivi sasa majesi ya UN yaliyopo Kongo yanafanya kazi chini ya kibali namba sita cha UN ambacho kinawataka wao kulinda amani tu, tunaomba katibu mkuu wa umoja huo atoe kibali namba saba ili majeshi hayo yapambane na waasi wa M23 na kuwaondoa.”

Membe alisema kuwa hivi sasa Serikali inasikitishwa kwa kushindwa kwa majeshi ya UN kuwazuia waasi wa M23 wasiteke mji wa Goma kwani kitendo hicho kinawapa nguvu waasi kuendelea na mapambano.

“Tunawataka waasi wote waiachie Goma kwa kuwa kilichotokea hakikubaliki, tunasikitika vikosi vya UN kushindwa kuzuia hilo, tunamuomba katibu mkuu wa UN atoe kibali kuruhusu wanajeshi wake wapambane ili kuzuia waasi wasiendelee na vita,” alisema Membe na kuongeza;

“Hatukubaliani na utekaji huo na kwamba kama wakiendelea na kuiteka Bukavu, tutapata wakimbizi wengi kutoka Kongo.”

Alisema wakati Serikali ya Tanzania ikitoa tamko lake kuhusu waasi hao leo viongozi wa nchi za maziwa makuu watakutana nchini Uganda na kufanya mazungumzo ambayo yatatoa uamuzi mgumu kama UN haitaruhusu majeshi yake au ya maziwa makuu kuingilia kati vita hivyo.

“Kesho (leo) na keshokutwa (kesho) uamuzi mgumu utatolewa ambao utalitatua tatizo la Kongo moja kwa moja,” alisema Waziri Membe na kuongeza;

“Tunailaumu UN kwa kutokuchukua maamuzi hayo magumu ya kuweza kuzuia vita nchini Kongo.”
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: