BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

UMOJA WA MATAIFA WASHTUSHWA NA HALI YA USALAMA NCHINI DRC.

Raia wakiwa wamejikusanya kwenye moja ya kifaru kilichotelekezwa na wanajeshi waliokimbia mji wa Goma Raia wakiwa wamejikusanya kwenye moja ya kifaru kilichotelekezwa na wanajeshi waliokimbia mji wa Goma.

UMOJA wa Mataifa umeelezea kushtushwa na hali ya mambo Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mara baada ya kushuhudia maelfu ya raia wakikimbia makazi yao kufuatia kusonga mbele kwa waasi na kuteka miji kadhaa katika taifa hilo,na kutoa wito wa msaada kwa wale walioathirika na ghasia.DRC president Joseph Kabila.

 Na katika kile kinachotajwa kuwa operesheni kubwa ya kwanza katika shughuli zake za kulinda amani, Umoja wa mataifa umesema kuwa unatazamia kutumia ndege zisizokuwa na marubani kufuatilia mapigano kati ya jeshi na waasi wa M23.

Viongozi wa ukanda wa maziwa makuu wanajielekeza jijini Kampala hii leo kwa ajili ya mkutano kuhusu mgogoro wa karibuni huko Masharaiki mwa DRC eneo lenye utajiri wa madini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: