BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WANANCHI WA ILALA WATAKA SIKU YA IJUMA IWE SIKU YA MAPUMZIKO.

WANANCHI wa Wilaya ya Ilala  Dar es Salaam,wamesema kuwa katiba itakayopatikana iruhusu siku ya ijumaa iwe siku ya mapumziko.

Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti mbele viongozi wa Tume ya Kukusanya Maoni, walisema kwamba siku hiyo iwe rasmi ya mapumziko kwa kuwa waumini wa  dini ya kiislamu wanatakiwa wawe kwenye ibada na siyo kazini.

Mkazi wa Kata ya Jangwani,Rashidi Musa alisema  katiba ikiruhusu siku hiyo iwe siku ya mapumziko itatoa fursa kwa waumini wa dini hiyo kwenda kwenye ibada kwa wakati.

Musa alisema watu wanapokuwa kazini wanabanwa na kazi hivyo wanashindwa kwenda kwenye ibada matokeo yake kila ikifika siku hiyo anakosa nafasi.

“Ile siku iheshimiwe iwe kama siku ya Jumamosi na Jumapili kwa nini siku hii ikifika watu wengine wanafanya kazi nusu siku na wengine wanafanya kazi siku nzima ambapo wanakosa muda wa kwenda kwenye ibada ya Ijumaa”alisema Musa.

Naye Mkazi wa Kata ya Gongolamboto, Gaudensia Busta alisema katiba itakayoundwa iseme kuwa wafungwa wanaotumikia vifungo wawe wazalishaji wakuu wanapokuwa magerezani.

Alisema utakuta wafungwa wanarundikana magerezani wakati serikali ilitakiwa kuwatumia hao katika uzalishaji kama kulima mazao mbalimbali kwa ajili ya chakula kiweze kupelekwa hospitalini na magerezani.

“Kama Serikali itawatumia wafungwa watumike kama wazalishaji wakuu wanapokuwa magerezani, nina imani wataweza kulima mazao mbalimbali na kupelekwa hospitalini ili chakula hiki kiwasaidie wagonjwa ambao hawana ndugu”alisema Busta
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: