BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WANNE WAFARIKI DUNIA KARIBU NA MGAHAWA WA THE VILLAGE MJINI MOGADISHU NCHINI SOMALIA.

 Polisi wa Somalia wakisaidia jeruhi katika shambulio la Septemba
WATU zaidi ya wanne wameuwawa na wengine 10 kujeruhiwa katika shambulio dhidi ya mkahawa mjini Mogadishu, Somalia.

Mwandishi wa BBC mjini humo anasema kumetokea miripuko miwili mikubwa nje ya mkahawa huo uitwao "The Village", katika mtaa wa Hodan, kati-kati ya mji.

Walioshuhudia tukio hilo wanasema mabomu yaliripuliwa na watu waliojitolea mhanga.

Mwezi wa Septemba watu 14 walikufa kwenye shambulio katika mkahawa mwengine mjini Mogadishu wa tajiri huyo-huyo.

Mwandishi wa BBC anakumbusha kuwa mashambulio kama hayo hufanywa mara kwa mara, na baadhi yao ni vitendo vya kundi la wapiganaji wa Kiislamu, al-Shabaab, ambao bado wanadhibiti sehemu kubwa ya nchi.

Mashambulio mengine hufanywa na magengi ya wahalifu na wanamgambo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: