BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WATU 13 AKIWEMO MKUU WA ZAMANI WA HUDUMA ZA KIINTELIJENSIA WASHIKILIWA SUDAN KWA NJAMA ZA KUVURUGA AMANI.

Mkuu wa zamani wa huduma za intelijensia nchini Sudani Salah Gosh 
Mkuu wa zamani wa huduma za intelijensia nchini Sudani Salah Gosh.  

WATU 13 wakiwemo maafisa wa jeshi na wa serikali wanashikiliwa nchini Sudani kwa madai ya kuhusika na mpango wa kuhatarisha amani nchini humo akiwemo aliyekuwa kiongozi mkuu wa muda mrefu wa huduma za kiintelijensia jenerali Salah Gosh.

Waziri wa habari nchini humo Ahmed Bilal Osman amethibitisha kushikiliwa kwa maafisa hao na kuwataja wengine kuwa ni jenerali Adil Al- Tayeb wa kitengo cha taifa cha huduma za kiintelijensia na usalama, brigedia Mohammed Ibrahim wa vikosi vya kijeshi vya Sudani.

Waziri Osman ameongeza kuwa wote waliokamatwa wanachunguzwa kuhusiana na mpango wa kuvuruga amani ambao awali ulipangwa kutekelezwa Novemba 15 lakini ulicheleweshwa hadi leo Alhamisi ambapo kitengo cha huduma za kiintelijensia kimearifu kuwa kimefanikiwa kuharibu njama hizo.

Kwa upande wa msemaji wa muungano wa vyama vya upinzani amekanusha kuhusika kwao katika jaribio la kuleta mabadiliko ya kisiasa kwa njia ya vurugu katika taifa ambalo limeshuhudia mapinduzi ya kijeshi saba au majaribio ya mapinduzi katika miaka 56 ya historia yake.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: