BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

PAPA FRANCIS 1 AENDELEA KUWASHANGAZA WENGI.

Kwa ufupi
Papa Francis ameadhimisha misa yake ya kwanza tangu alipochaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, huku akitoa hotuba ya dakika tano mbele ya waumini wa Parokia ya Mtakatifu Anna.
 Papa Francis 1 (kulia) akiwa na mtangulizi wake Papa mstaafu Benendict XVI.

Vatican City. 
PAPA Francis ameadhimisha misa yake ya kwanza tangu alipochaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, huku akitoa hotuba ya dakika tano mbele ya waumini wa Parokia ya Mtakatifu Anna.

Jana, katika mahubiri yake mafupi, Papa Francis alishangaza wengi kwa kueleza kuwa binadamu hawana budi kusameheana, kama ambavyo Mungu amekuwa mwenye huruma kwa wanadamu.
Awali, Papa alijitokeza hadharani katika lango kuu la kuingilia kanisa hilo la parokia akiwa amevaa kanzu nyeupe, viatu vyeusi, kuwapungia mkono watu wote, kisha kupeana nao mikono.
Kisha, alibusu, kuwashika mabegani watoto na kueleza kuwa jukumu la binadamu ni kupendana.
“Ningependa sisi sote tuwe na ujasiri wa kutembea katika uwepo wa Mungu,” alisema Papa Francis kwa Kilatini.
Mapema, Papa alifanya maombi binafsi katika Kanisa Kuu la Santa Maria Maggiore na baadaye alikutana na watoto na wasafiri waliokwenda kumsalimia.
Papa, pia ameanza kazi ya uteuzi wa maofisa wa juu wa Vatican, ingawa orodha hiyo haijakamilika wala kuwekwa wazi.
Jumatano usiku muda mfupi baada ya kuchaguliwa kwake, aliusalimia umati wa watu waliofurika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro akitoa wito wa unyenyekevu na kuwaomba waumini wamwombee baraka kabla yeye hajawabariki.
Alhamisi, Papa Francis alirudi kwenye makazi ya watumishi yaliyopo mjini Rome alipokuwa akiishi mbele ya jengo la mikutano ulimofanyika uchaguzi uliomweka madarakani.
“Alifungasha mizigo yake na kwenda kulipia chumba alichofikia ili kuwa mfano bora.
“Pia, alivunja utamaduni wa kwenda kuwasubiri makardinali waliokwenda kumpa pongezi, badala ya kukaa kwenye kiti cha enzi,” alisema msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi.
Ijumaa alikutana na makardinali 106 wakiwamo wale ambao hawakuingia kwenye mkutano wa uchaguzi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: