BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KIZAZI HIKI CHA WASANN KIEPUKWE.

MWANANCHI. 
MAONI YA MHARIRI:
KATIKATI ya wiki hii, sanaa ya muziki ilipokea kwa huzuni taarifa za kifo cha mwanamuziki Albert Mangwea aliyefariki nchini Afrika Kusini alikokwenda kwa shughuli za muziki.
Marehemu Albert Mangwea.Bi Kidude
Bi Kidude playing in Nairobi, Kenya, in 2006.

KIFO cha Mangwea, msanii wa muziki wa Bongo Fleva maarufu kama Ngwair kimekuja mwezi mmoja tangu kifo cha msanii mkongwe na alama ya muziki wa mwambao, Bi Kidude.

Misiba hii mfululizo ni wazi imepoteza watu muhimu katika sanaa ya muziki, ambao hakika walik
uwa sehemu ya mafanikio tunayoshuhudia kwenye fani hiyo kwa sasa.

Kifo cha msanii Ngweair kimeacha maswali mengi miongoni mwa wadau hasa kufuatia kutojulikana chanzo halisi cha kifo chake kilichotokea katika mazingira ya utata.

Utata unakuja baada ya kuelezwa mengi kuhusu kifo chake, ambacho kimehusishwa na ulevi wa pombe na matumizi ya dawa za kulevya kupindukia.

Kulikuwa na taarifa iliyochapishwa kwenye mitandao ilieleza sababu ya kifo cha msanii, kwamba matumizi ya pombe, bangi na dawa za kulevya ndiyo sababu ya kifo chake.

Ingawa taarifa hiyo haikuwa rasmi kwa maana ya kuthibitishwa na familia ya marehemu, lakini hatunyimwi nafasi ya kuwapa ushauri wasanii wetu, ambao wengi ni vijana wadogo kwa matumizi ya dawa za kulevya.

Ni kawaida kusikia wasanii kujihusisha na vitendo visivyokubalika mbele ya jamii, kwa mfano ulevi, uhuni, umalaya, matumizi ya dawa za kulevya, bangi na mambo mengine yasiyofaa.

Namna yoyote ya kwenda kinyume na maadili yanayokubalika mbele ya jamii, kunaweza kumchafua msanii ambaye anapaswa kuwa alama ya kuelimisha na kukosoa kupitia sanaa ya muziki.

Lakini tunachokishuhudia kwa baadhi ya wasanii wetu ni kwenda kinyume na mahitaji ya kuistawisha jamii kwa kujihusisha na matendo mabaya yanayowachafua hata wao wenyewe.

Tuna ushahidi mkubwa jinsi wasanii wanavyojihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya, ulevi, bangi, umalaya na uhuni. Matendo haya siyo tu yanamchafua msanii, bali pia hayana mashiko mbele ya jamii.

Wasanii wanapaswa kutambua mchango wao katika jamii na kuwa mfano wa kuigwa na siyo kinyume chake kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia katika fani ya muziki hapa nchini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: