BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HAYA NDIYO MAMBO YANATOTAKIWA KUFANYA NA WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU KATIKA KIPINDI CHA MWENZI WA RAMADHANI NA KUENDELEA.


MWEZI Mtukufu wa Ramadhani umeandama jana kuashiria kuanza kwa Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao ni mojawapo ya nguzo tano za dini ya kiislamu.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema jana: "kuwa lulingana na kalenda ya dini ya Kiislamu na mwezi umeandama hivyo (leo)  Jumatano waumini wa dini ye kiislamu wapo katika funga.”

Sheikh huyo aliwataka waumini wa dini hiyo kushika msingi ya dini na kutekeleza yote yaliyo mema ambayo yanahimizwa wakati wa mfungo.

Pia Sheikh Salum aliwataka wafanyabiashara kuacha kuutumia Mwezi Mtukufu kupandisha bei za vyak
ula na badala yake waongeze huruma kwa kujitahidi kuvuna thawabu badala ya dhambi katika kipindi hiki. 

“Pamoja na kuwa tunaingia katika mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kila mmoja ajitafakari kwanza kuzidisha ibada, kufanya matendo mema na zaidi ni kudumisha amani ya nchi yetu…lazima kuilinda na kuitetea amani yetu kwani ni bora kuilinda kuliko kuipoteza.”
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: