Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini Nelson Mandela akifurahia jambo na wajukuu zake wakati alipokuwa na afya njema.
AFRIKA YA KUSINI.
WAZEE wa kimila wa Kabila la Xhosa, wamesema kuwa mgogoro kati ya Mandla na wanafamilia wengine wa Mandela wa kufukua mabaki ya miili ya watoto wa Rais huyo wa zamani, umeishusha hadhi mila na tamaduni za Kiafrika.
WAZEE wa kimila wa Kabila la Xhosa, wamesema kuwa mgogoro kati ya Mandla na wanafamilia wengine wa Mandela wa kufukua mabaki ya miili ya watoto wa Rais huyo wa zamani, umeishusha hadhi mila na tamaduni za Kiafrika.
Phathekile Holomisa, kiongozi mkuu wa chama cha
kimila cha Afrika Kusini alikaririwa akiukosoa vikali uamuzi huo wa
kuipeleka kesi hiyo mahakamani badala ya kuutatua kwa mkutano wa kimila
au Ibhunga.
“Ingekuwa ni vyema kama wangeifukua miili hiyo
kitamaduni kwa kuwaita wazee wa kimila wa Kabila la Mad
iba badala ya kutumia mahakama ambayo sheria zake ni za kigeni na si za kwetu,”alisema Holomisa.
iba badala ya kutumia mahakama ambayo sheria zake ni za kigeni na si za kwetu,”alisema Holomisa.
Holomisa aliongeza kuwa jambo baya zaidi ambalo
wanafamilia hao wamefanya ni kushindwa hata kuwaita wazee wa kimila
kusali na kuzungumza na wazee wa jadi ambao ni wamiliki wa mabaki hayo.
“Ili ufukue miili na kuizika upya unahitaji kuchinja na kutoa kafara,kutengeneza pombe kwa mizimu,kuiomba na kuieleza kwa nini unahamisha mabaki ya miili hiyo hadi ikubali,”alisema Holomisa.
“Ili ufukue miili na kuizika upya unahitaji kuchinja na kutoa kafara,kutengeneza pombe kwa mizimu,kuiomba na kuieleza kwa nini unahamisha mabaki ya miili hiyo hadi ikubali,”alisema Holomisa.
Wakati mgogoro wa wanafamilia ya Rais wa zamani wa
Afrika Kusini, Nelson Mandela kuhusu mahali pa kuzika miili ya watoto
wa Rais huyo ukihitimishwa na mahakama, madaktari wanaomtibu Madiba
wamethibitisha kuwa kiongozi huyo hapumui kwa msaada wa mashine.
Ofisi ya Rais, Afrika Kusini ilithibitisha hilo
juzi na kusema kuwa Rais Jacob Zuma alimtembelea Mandela Alhamisi mchana
na kusema kuwa hali yake ni mbaya lakini hapumui kwa msaada wa mashine
kama baadhi ya wanafamilia wa Mandela walivyowahi kukaririwa wakisema.
“Tunathibitisha kauli hii kwa mara nyingine kuwa
Rais Zuma alimtembelea Mandela hospitalini na aliweza kuona hali yake
ilivyo kwa sasa,” alisema msemaji wa Rais Zuma, Mac Maharaj.
Msemaji huyo alisema Mandela anatibiwa na jopo la
madaktari bingwa kutoka Jeshi la Afrika Kusini,madaktari binafsi,wa umma
na madaktari bingwa kutoka Vyuo Vikuu nchini humo.
Wanafamilia ya Tata Mandela waumbuana
Mthatha.Ugomvi ndani ya familia ya Rais mstaafu wa
Afrika Kusini, Nelson Mandela umegeuka kuwa mfululizo wa mivutano ndani
ya ukoo, ambapo juzi Mandla alimtuhumu mwanafamilia mwenzake kwa uzinzi
na ulafi wa mali za babu yake.
Akizungumza kwenye televisheni katika matangazo
yaliyorushwa moja kwa moja na kutazamwa na mamilioni ya watu, Mandla
aliuthibitisha umma kwamba mtoto wake wa kiume, Zanethemba ni mtoto wa
kaka yake Mbuso, baada ya kufanya uzinzi na mkewe (Mandla), Anais
Grimaud ambaye amemtaliki.
“Mbuso alimpa ujauzito mke wangu,”alidai Mandla alipozungumza kwenye televisheni akiwa kijijini kwake Mvezo.
CHANZO MWANANCHI
CHANZO MWANANCHI

0 comments:
Post a Comment