BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JESHI LA POLISI LAINGIA LAWAMANI KWA MADAI KUMSHAMBULIA MWANANCHI NA KUMVUNJA MKONO.


Omary Hamis akionyesha jeraha alilopata baada ya kudaiwa kupokea kipigo kutoka kwa askari wa jeshi la polisi mkoani Ruvuma.
Joseph Mwambije, Songea
JESHI la polisi mkoani Ruvuma limeingia lawamani baada ya askari wake kudaiwa kumshambulia, Omary Hamis mkazi wa Mfaranyaki Makaburini na kumvunja mara mbili mkono wa kulia na bega la kushoto na kumjeruhi maeneo mbalim
bali ya mwili wake baada ya kupigana na mkewe ambapo amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma kwa matibabu.

Askari wa jeshi hilo wanadaiwa kumshambulia Omary Hamis mkazi wa Mfaranyaki Songea huku watoto wake wakishuhudia na kumpiga kwa virungu na kumvunja mkono wa  kulia na bega la kushoto na kumsababishia majeraha mbambali kwenye mwili wake baada ya  mwananchi huyo kupigana na mkewe aliyewapigia simu polisi kutokana ugomvi waliokuwa nao mke na mume. 

Mtoto wa Abubakary Omary mwenye miaka 11 alishudia tukio hilo wakati baba yake ikipata kipigo hicho.

Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma, George Chiposi alipofuatwa na ITV ofisini kwake kwa siku mbili mfululizo aweze kuzungumzia tukio hilo hakuweza kupatikana na alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi na kuelezwa kuhusiana na tukio hilo hakusema chohote na kukata simu.
Mtoto wa Bwana Omary Hamis akiongea na ITV.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: