BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

REDIO IMAN, KWA-NEEMA FM SASA KUPASUA ANGA AGOSTI 27/2013, NI BAADA YA KUTUMIKIA KIFUNGO CHA MIEZI SITA.

Mwenyekiti wa Islamic Foundation Br Arif Nahdi akihojiwa na Radio MuM juu ya ujio wa Radio Imaan.
Mtaalam wa Mitambo wa Radio Imaan na Tv Imaan Muhammad Maembe akimuelekeza Mwenyekiti wa Islamic Foundation Br Arif Nahadi mitambo inavyofanya kazi katika jengo jipya la makao makuu ya Radio na Tv Imaan

Hizi ndizo sababu za kufungiwa Radio Imani na Radio Kwa Neema.

KAMATI ya Maadili ya Utangazaji nchini imevifungia vituo viwili vya radio pamoja na kukipiga faini ya Sh mil 5, kituo cha Clouds FM kutokana na kukiuka maadili ya utangazaji.

Vituo hivyo viwili vya redio ambavyo vyote kwa pamoja vimefungiwa kutorusha matangazo yake kuanzia leo kwa miezi sita ni pamoja na Imani FM cha Morogoro na  Kwa-Neema FM kilichopo mkoani Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Walter Bgoya alisema Kituo cha Clouds FM kimetakiwa kufuta kipindi chake cha Jicho la Ng'ombe mara moja pamoja na kulipa faini ya sh. milioni 5.
 
Akifafanua zaidi Makamu Mwenyekiti huyo alisema vituo vya Imani FM na Kwa-Neema vimefungiwa kwa kosa la kufanya kazi zao kwa uchochezi jambo ambalo ni kinyume cha maadili ya tasnia ya utangazaji. Kituo cha Clouds FM kimetakiwa kutoanzisha kipengele (segment) nyingine inayofanana na Jicho la Ng'ombe iliyo katika kipindi chao cha asubuhi cha ‘Power breakfast’.

Kituo cha Imani FM kinadaiwa kufanya uchochezi kwa wananchi juu ya suala la sensa ya watu na makazi huku kile cha Kwa-Neema kufanya uchochezi juu ya mgogoro wa uchinjaji wanyama kwa Waislamu na Wakristu mkoani Geita.

Hata hivyo Kamati ya Maadili imeweka mlango wazi kwa vituo hivyo kukata rufaa endapo havikuridhika na adhabu vilivyo pewa kutokana na makosa vinao daiwa 
kufanya.
 
Kamati Imevitaka vyombo vyote vya habari kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni Sheria na maadili ya tasnia hiyo ili kuepuka kuzua migogoro kwa wananchi ambao wamekuwa wakiviamini vituo hivyo.
 
Hata hivyo mara baada ya ujumbe wa kamati hiyo kumaliza kusoma adhabu hizo kwa waandishi wa habari haukuruhusu maswali kwa waandishi wa habari, hivyo waandishi kubaki wameduwaa.
 
Akizungumza kwa njia ya simu mkurugenzi wa Clouds FM Ruge Mutahaba alisema haoni tatizo kwa viongozi hao kufikia hatua hiyo kwani wanafanya kazi yao, lakini kwakuwa wamepewa nafasi ya kukata rufaa watajipanga na kuenda kuwaelewesha maana na umuhimu wa waliyokuwa wakiyarusha katika sehemu (segment) ya jicho la ngombe iliyo katika kipindi chao cha asubuhi.
Sababu za kufungiwa:
-Kwa Neema FM Mwanza: Sababu ni kushabikia maswala ya uchinjaji Mwanza
- Radio Iman FM Morogoro: Kushabikia watu kutoshiriki Sensa 2012
- Clouds FM: Kushabikia ushoga & kuendesha kipindi kisichofuata maadili (Jicho la Ng’ombe). 
Ambapo kifungo hicho kilianza rasmi Tar 26 feb 2013.
 
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: