BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NAPE NNAUYE AMSHAWISHI RAIS JAKAYA KIKWETE KUWAWAJIBISHA AKINA DK SHUKURU KAWAMBWA, CHIZA NA MALIMA KISA WAMESHINDWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO.

MawaziriMAWAZIRI watatu wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete wapo katika wakati mgumu baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),
 
Nape Nnauye, kutangaza rasmi kuwa atahakikisha wanachukuliwa hatua za kuwajibishwa kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yao. 
 
Wakati Nape akitaka mawaziri hao watimuliwe, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulhaman Kinana, amesema kuwa mawaziri hao watawekwa kiti moto katika kikao kijacho cha Kamati
Kuu (CC), kwa lengo la kueleza ni hatua gani wanachukua katika
kushughulikia matatizo ya Watanzania.



Mawaziri hao ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi
Christopher Chiza,  Naibu wake, Adamu Malima  na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa ambaye ametajwa kuwa sehemu ya matatizo katika kila wizara anayopewa kuiongoza. TANZANIA DAIMA.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: