BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HATARI YA KUVUNJIKA KWA KATIBA YAFICHUKA.

Kanuni za Katiba ni kanuni ambazo zimepitishwa baada ya kupatikana kwa sheria, hivyo wanatakiwa kwanza ama kurejea katika Bunge la Jamhuri.

Dar es Salaam.
 

Wakati Bunge Maalumu la Katiba linakusudia kufanyia marekebisho kanuni zake ili kuwabana wajumbe wa Bunge hilo ambao wamesusia kushiriki mchakato wa Katiba, wanasheria, wasomi na wanaharakati wamepinga dhamira hiyo wakisema itasababisha kuvunjwa kwa Katiba.


Wajumbe wanaolengwa katika marekebisho hayo ni wale wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutoka Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na baadhi ya wajumbe kutoka Kundi la 201 walioteuliwa na Rais.


Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki alisema mabadiliko yanayokusudiwa kufanywa yatahusisha masuala ya nidhamu, yakiwamo fujo na utoro, mambo ambayo hivi sasa hayawezi kudhibitiwa moja kwa moja na mwenyekiti wa Bunge hilo.


Sitta alikuwa akitoa ufafanuzi wa taarifa iliyotolewa na ofisi yake juzi na kusomwa mbele ya waandishi wa habari na Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad, ikieleza maazimio ya kikao cha usuluhishi alichokuwa amekiitisha kwa ajili ya kutanzua mzozo unaotishia kukwamisha mchakato wa Katiba Mpya.


Taarifa hiyo ilisema kitendo cha Ukawa kuendelea kususia Bunge, kinapuuza wito wa jamii kupitia makundi mbalimbali pamoja na madhehebu ya dini na juhudi za usuluhishi za kutaka kuwezesha vikao vya Bunge hilo viendelee.


Ukawa walitoka bungeni siku chache kabla ya kuahirishwa kwa awamu ya kwanza ya Bunge Maalumu Aprili 16 mwaka huu, kwa madai kwamba CCM kinatumia wingi wa wajumbe wake kutaka kufutwa kwa baadhi ya mapendekezo ya wananchi yaliyomo kwenye Rasimu ya Katiba.


Tayari Mwenyekiti Ukawa, Freeman Mbowe na Mwenyekiti Mwenza, Profesa Ibrahim Lipumba wamesisitiza kuwa hawatarejea bungeni hata kama Bunge litafanyia marekebisho kanuni ili ziwabane Ukawa.


Profesa Maina
Mtaalamu wa Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Chris Peter Maina alisema kama wanataka kufanyia mabadiliko kanuni, kinachotakiwa kufanyika kwanza ni kubadili sheria ya mabadiliko ya Katiba ili kanuni zilizokusudiwa kufanyiwa marekebisho zisiwe juu ya sheria.


“Kanuni za Katiba ni kanuni ambazo zimepitishwa baada ya kupatikana kwa sheria, hivyo wanatakiwa kwanza ama kurejea katika Bunge la Jamhuri kufanya marekebisho ya sheria, kisha ndiyo wafanye hayo marekebisho wanayoyataka ya kanuni,” alisema Profesa Maina.


Aliongeza: “Kinachotakiwa hapa ni watu kuheshimu sheria kama tunataka mchakato huu umalizike salama na tupate katiba bora na yenye kuweka mbele masilahi ya taifa.”


Profesa Shumbusho
Profesa wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, George Shumbusho alisema jinsi mchakato ulipofikia hakuna haja ya kuupeleka haraka na kinachotakiwa ni kuusimamisha na kufanya marekebisho kwa Katiba ya sasa.


“Sijui haraka hizi za nini. Hakuna haja ya kufanya marekebisho ya kanuni, tuifanyie marekebisho Katiba ya sasa hasa vipengele vya uwepo wa tume huru ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015 na baada ya hapo sasa ndipo mchakato huu uendelee tena, lakini sasa umekwama,” alisema Profesa Shumbusho.


Aliongeza: “Kama Ukawa wametoka tatizo siyo kubadili kanuni tunatakiwa kupata majibu kwa nini wametoka na katiba bora haiji kwa kubadili kanuni.”


Profesa Shumbusho alisisitiza kuwa mchakato ulipofikia hakuna haja ya kuupeleka haraka na kinachotakiwa ni kuusimamisha na kufanya marekebisho kwa Katiba ya sasa.


“Sijui haraka hizi za nini, hakuna haja ya kufanya marekebisho ya kanuni, tuifanyie marekebisho Katiba ya sasa hasa vipengele vya uwepo wa tume huru ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015 na baada ya hapo sasa ndipo mchakato huu uendelee tena, lakini sasa umekwama,” alisema Profesa Shumbusho.


Aliongeza: “Kama Ukawa wametoka tatizo siyo kubadili kanuni tunatakiwa kupata majibu kwa nini wametoka na katiba bora haiji kwa kubadili kanuni.”


Maria Kashondo
Maria Kashondo aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema Bunge hilo linachokifanya sasa ni batili kwa sababu idadi ya wajumbe waliobaki ndani ya Bunge hawakidhi akidi inavyotakiwa kisheria.


Alisema kosa lilianza kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano kufanya marekebisho ya sheria kuhusu ukomo wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, kwani ingekuwapo wajumbe wake wangekuwa wakifafanua baadhi ya vipengele vinavyoonekana kutokueleweka vizuri.


“Walirekebisha sheria ili Tume isiwepo, ingekuwapo haya yanayotokea yasingekuwapo. Lakini marekebisho yanayofanywa na Bunge hilo likiwa pungufu ni batili, hata yale yaliyokwishafanyika nayo ni batili,” alisema Kashonda.


Polepole
Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko Humphrey Polepole alisema Sitta anatakiwa kuwa kama baba katika familia kwamba mtoto anapokosea hutakiwi kumwadhibu bila kujua tatizo.


Alisema kama Ukawa wamegoma kufika meza ya majadiliano Sitta hakutakiwa kuwa na hasira alitakiwa kujishusha na kutumia busara na hekima kuwaita tena na wakigoma sasa wananchi wataona nani ni mkorofi.


“Kilichotokea ni kutibu matokeo badala ya kuangalia mzizi, tatizo lililopo katika Bunge Maalumu la Katiba linatakiwa kuangaliwa kwa mapana na si juu juu tu, kwani kama Tume nayo ingekuwa hivyo Rasimu iliyopo mezani isingepatikana,” alisema Polepole ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi za kiraia nchini.


Mandari
Mratibu wa Muungano wa Jinsia na Katiba wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (Tawla), Vicky Mandari alisema huwezi kufanya marekebisho ya kanuni bila kuanza na marekebisho ya sheria.


“Uroho wa madaraka ndiyo unatufikisha hapa. Kuna matatizo lukuki ya wananchi hasa miundombinu ya elimu, maji, afya hivyo wanatakiwa kujikita kujadili mambo haya na si kukimbilia kufanya marekebisho ya kanuni.”


“Bunge hilo linatakiwa kujua kwamba wao siyo wenye uamuzi wa mwisho, kwani hata wakifanya vipi bado wananchi ndiyo watakuwa na kauli ya mwisho kuhusu Katiba Mpya. Tunawaomba waweke mbele masilahi ya taifa kabla ya vyama vyao,” alisema Mandari.


Ngurumwa
Mratibu wa Mtandao wa Wapiganiaji wa Haki za Binadamu, Onesmo Ole Ngurumwa alisema katiba inavyoandaliwa inatakiwa kuyashirikisha makundi mbalimbali na ikitokea kundi moja likasusia mchakato huo, hautakiwi kuendelea kisheria, kwani utakuwa unakiuka Katiba ya nchi.


“Unapofanya marekebisho ya kanuni ni lazima zilingane na sheria. Huwezi kuwa na kanuni zilizo juu ya sheria, kwani wakifanya hivyo watasababisha vurugu kama zilizotokea kwa wenzetu kule Kenya,” alisema Ngurumwa.


Aliongeza: “Hapa mchakato umekwama na hakuna haja ya kubadili kanuni. Umefika wakati wa Rais Kikwete (Jakaya Kikwete) kama mwenyekiti wa chama chake (CCM) kuchukua uamuzi wenye kujali masilahi ya watu wote kwa kuukwamua mchakato huu, bila hivyo hakuna kitakachoendelea.”


Mkazi wa Kimara Dar es Salaam, Aivan Alfred alisema Julai 31 mwaka huu anakusudia kufungua kesi ya kupinga kuendelea na vikao vya Bunge Maalumu la Katiba kujadili Rasimu ya Katiba.


Alisema pingamizi hilo linatokana na Bunge hilo kujadili mambo ambayo ni kinyume na maoni yaliyotolewa na wananchi.


“Nitakwenda kusimama mahakamani kwa niaba ya Watanzania zaidi ya milioni 44.5 kupinga mjadala huo usiendelee.


“Hatuwezi kuacha wao wajadili mambo ambayo si maoni yetu. Hili suala la Serikali mbili halipo kwenye rasimu hata ukisoma sura ya kwanza hadi ya mwisho hakuna kitu kama hicho,” alisema Alfred.


Alisema taasisi na viongozi wa dini wamesema, lakini bado mambo yanaendeshwa kijanja janja tu, Ninasema sasa basi, kwa miaka 50 tumekuwa na Katiba waliyoitaka wao yenye viraka na upungufu lukuki, hivi sasa tunataka Katiba tunayoitaka sisi.”


Hamad Salim, Mhadhiri Chuo Kikuu Huria
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Hamad Salim alisema kinachotakiwa kufanyika kwanza kabla hata ya kuunda hizo kanuni ni makubaliano baina ya pande hizo mbili.


“Makubaliano ndiyo msingi wa kupata katiba tunayoitaka, lakini wanavyokimbilia kwenye masuala ya kanuni haifai. Ukiangalia wanaoenda kutunga kanuni ni wale wale ambao wamekuwa wakilinda masilahi yao wenyewe,” alisema Salim na kuongeza:


“Lakini hii hali ilianza kudhihirika tangu hapo awali mchakato huu ulipoanza. Tuliona kabisa hawa watu hawapo pale kwa ajili ya kutetea na kulinda masilahi ya wananchi bali masilahi yao wenyewe na hicho ndicho kinachoendelea sasa”


Alisema mambo yamekuwa yakipelekwa mbio mbio, hakuna ushirikishwaji wa wananchi ambao ni yakinifu wenye kuwapa elimu na ufafanuzi wa kila hatua ya mchakato kiundani kama inavyostahili.


Mhadhiri huyo alisema kama hata hizo kanuni zikiwekwa haziwezi kuwa tiba ya kupata suluhu na hatimaye kupata Katiba wanayoitaka Watanzania.


“Ni bora huu mchakato uvunjwe. Tusubiri uchaguzi ujao wa 2015 upite halafu mchakato uanze upya.”MWANANCHI

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: