BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAJAMBAZI WAMPORA MSALABA NA PETE KADINALI WA KANISA KATOLIKI.

Kadinali Dom Orani Tempesta alitawazwa na Papa Francis.

Watu waliokuwa wamejihami wamemuibia Askofu mkuu wa Rio de Janeiro nchini Brazil msalaba wake na pete

Kadinali, Dom Orani Tempesta, alikuwa njiani kuelekea kuhudhuria mkutano mjini alipovamiwa na majambazi hao.

Mmoja wa majambazi aliyekuwa na bunduki katika kanisa, alimfahamu kadinali huyo na kumuomba msamaha.

ParĂ³quia de Pacajus, Pacajus, Dom Orani, Catequista 
Hata hivyo, hilo halikushutua genge hilo ambalo liliendleea kumpora kadinali huyo, na hata nusura wampore gari lake.

Vitu vilivyoibwa vilipatikana baadaye.
Hakuna aliyejeruhiwa kwenye tukio hilo, ambalo lilifanyiika Jumatatu jioni katika mtaa wa Santa Teresa.

Mwandishi wa BBC Gary Duffy, anasema kuwa visa vya wizi hutokea mara kwa mara katika mtaa huo wenye shughuli nyingi za kitalii na kwamba visa hivyo vimekuwa vikiongezeka sana mwaka huu.

Mwanafunzi wa dini pamoja na mpiga picha mmoja waliokuwa kwenye gari na kadinali huyo pia waliporwa.

Licha ya tukio hilo, kadinali aliendelea na shughuli zake huku mwanafunzi na mpiga picha wakienda kuripoti kwa polisi.

Pete ya kadinali na msalaba, vilipatikana pamoja na simu yake ya mkononi

Hata hivyo, vifaa vya mpiga picha havijapatikana.

Dom Orani Tempesta alitawazwa kama kadinali na Papa Francis mapema mwaka huu.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: