BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MATOKEO YA MKOA WA DAR ES SALAAM YANATOSHA KUMTANGAZA DK JOHN MAGUFULI MSHINDI WA URAIS KATIKA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 25 TANZANIA


Na Marthia Canal Wa Iramba.
MATOKEO YA MKOA WA DSM YANATOSHA KUMTANGAZA MAGUFULI MSHINDI.
Matokeo ya mkoa wa Daresalam yananifurahisha kuliko yanavyowafurahisha UKAWA. Wamekuwa wakiyashangilia ila wanashindwa kuyaangalia kwa jicho la kitafiti. Ngoja niwaonyeshe kitu hapa.

Ipo hivi Mkoa wa Daresalam ndio mkoa uliokuwa na wapiga kura wengi kuliko mikoa yote tanzania walikuwa wamejiandikisha watu 2,000,000+ hakuna mkoa uliokuwa na idadi kubwa ya wapiga kura namna hii hapa nchini hilo lipo wazi.

Wagombea wote walikuwa wanaujua mtaji huu hivyo waliwekeza zaidi kwenye mkoa huu. Ukawa ndio waliokuwa wamewekeza zaidi kwenye mkoa huu ila matokeo ya uchaguzi huu hauendani na uwekezaji waliouwekeza. Kwa maana hiyo Daresalam ni mkoa ambao ulikuwa unategemewa sana na ukawa na Lowassa kila weekend alikuwa anarudi Dar kufanya Kampeni.

Ikumbukwe kwamba mpaka matokeo ya mchana wa leo kutoka tume Magufuli alikuwa na kura 1,687, 752 huku Lowassa akiwa na kura 1,215,555 hapa Magufuli amemzidi Lowassa kwa kura 472,198. Nilikuwa nasubiri mkoa wa Daresalam kama wanaweza kulipunguza hili gape wafuasi wamebaki kushangilia kina Kubenea bila kujua matokeo yale yamebeba nini. 

Ngome pekee waliyobaki nayo Chadema ni Mkoa wa Kilimanjaro na Arusha tu hii ni hatari kwao.
Sassa tuyachambue matokeo ya mkoa wa Daresalam ili uelewe naongea nini. Mkoa wa DSM ulikuwa na majimbo 10 hapa nitatoa mchanganua ambao Ukawa wamenyakua majimbo na jimbo moja tu la CCM, Yale mengine ya ambako CCM imeshinda sitayazungumzia kwa kuwapendelea kabisa wana Ukawa hayo sitayaweka hapa , kama wapiga kura zaa wabunge walimchagua pia raisi mambo yangekuwa hivi:-

1.TEMEKE:- UKAWA Kura 103,231 CCM kura 97,555
2. KAWE: - UKAWA Kura 96,432 CCM Kura 83,061
3. UBUNGO:- UKAWA Kura 87,606 CCM Kura 59,514
4. ILALA:- UKAWA Kura 32,533 CCM Kura 35,818
5. KIBAMBA:- UKAWA Kura 79,274 CCM Kura 55,410

Ukichukua jumla ya Kura za UKAWA hapo unapata jumla ya kura 399,076 na za CCM kura 367,830 ukitafuta tofauti ya kura kwa majimbo haya utaona UKAWA wanazidio la kura 31,346 tu kwa majimbo yote matano hapo juu yamebaki majimbo mengine 5 ambayo 3 CCM wameyashikilia nayo ni Kigamboni, segerea, na Kinondoni.

Ukichkua 31,346 ya zidio la kura hizi za ukawa ukajumlisha na zile za Lowassa hadi mchana wa leo utapata kura 1,246,801 Magufuli muachie zile zile za mchana 1,687, 752 ukitoa hapo Magufuli anakuwa na zidio la kura 440,951. Narudia hapa sijaweka majimbo 3 mengine waliyoshinda ccm nimeweka moja tu la Ilala.

Kama Ukawa wameshindwa kutumia fursa ya mkoa huo wa Daresalam wanasubiri ushindi wapi? Arusha na Kilimanjaro inaweza kushindana na Kanda ya ziwa? 

Kuna uwezakano mkubwa sana kuwa mtu alimchagua Kubenea ila uraisi akampa Magufuli hilo linawezekana hivyo tarajia makubwa hapa inawezekana Magufuli akawa na kura nyingi kuliko Lowassa kwenye Mkoa huu. 

Ukawa hapa mmepigwa jipangeni kwa 2020 kwani hata huko Arusha na Kilimanjaro mmekabana sana.

Hiki ni kichapo kwa wale wazee wa statistics watanielewa hapa nikipata matokeo ya Arusha tu nitakuwa nimeshajua Magufuli atashinda kwa Asilimia ngapi.
KUTOKA MITANDAO YA KIJAMII OKTOBA 29, 2015
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: