BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAAJABU YALIYOJAA VATICAN CITY NDIO HAYA.

Na Geofrey Chambua.
VATICAN ni nchi yaliko makao makuu ya Kanisa Katoliki.
Nchi hii ina mambo mengi ambayo yapo tofauti na nchi nyingine duniani. Baadhi ya mambo machache ni haya yafuatayo:

1. Ndio nchi ndogo kuliko zote duniani ikiwa na ukubwa wa 44 hectare(110 acres). 


Ikiwa na jumla ya watu 800 kwa mujibu wa data za hivi karibuni na hadi kufikia mwaka 2011, nchi nzima ilikua na WANAWAKE 32 tu na wote wanajulikana kazi zao na wanapoishi ( According to the Herald Sun, there were "only 32 female citizens" residing by 2011). 

Karibu nusu ya Raia wake wanaishi nje ya nchi wakiwemo mabalozi waliotapakaa karibu kote duniani ingawa Mabalozi wa nchi za Kigeni kwa Vatican huishi katika Jiji la Roma

2. Ilikuwa nchi kamili Feb 11, 1929 baada ya Benitto Mussolini(kwa niaba ya Mfalme wa Italy) kutiliana saini na Pietro Gasparri(kwa niaba ya Pope) hivyo kuwa nchi huru ndani ya jiji la Roma.

3. Kiongozi wa nchi hii (Pope) ndie kiongozi pekee anaeongoza nchi kifalme baada kuchaguliwa kwa kupigiwa kura. Papa aliwahi kuishi miaka 60 ndani ya Vatican bila KUSAFIRI NJE ya nchi. Askari wote wanaomlinda Pope wana asili ya Uswis na hujulikana kama Swiss Guard

4. Ni nchi pekee yenye waumini wa dini moja huku 99% kati yao wakiwa ni wasomi wa elimu ya juu na 75% ya Raia wake wamepitia mafunzo ya kishushushu. Ni moja ya nchi zenye Intelejensia ya hali ya juu sana duniani

5. Inasemekana kanisa la St.Peter yalipo makao ya Papa huwa linaongezeka ukubwa kutokana na wingi wa watu,Ni sehemu pekee ambapo karibu la Mtume Petro linapatikana (St Peter's Basilika)

6. Benki ya Vatikani ambayo pia hujulikana kwa jina la Institute for Works of Religion inafanya shughuli za kibenki duniani kote ambayo ATM zake zina maelekezo kwa Kilatini tu.

7. Ni nchi pekee duniani isiyokuwa na mapato yatokanayo na kodi. vyanzo vikuu vya mapato ni mauzo ya stempu na viingilio kwenye majumba ya kale toka kwa watalii kadhalika wafanyakazi wote ndani ya Vatican hawatozwi kodi yoyote

8. Ni mojawapo ya nchi mbili duniani ambazo hazina sheria ya talaka nyingine ni Filipine.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: