BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NCHI YA CHINA YAZINDUA BASI LENYE UWEZO WA MAGARI MADOGO KUPITA UVUNGUNI MWAKE


Basi la kipekee lenye urefu wa mita mbili juu linaloruhusu magari ya kibinafsi kupitia mvunguni mwake limefanyiwa majaribio katika mji waHebei kaskazini mwa Uchina.

Basi hilo linalopigiwa upatu kutatua kabisa tatizo la usafirishaji wa watu katika miji yenye idadi kubwa ya watu ama Transit Elevated Bus (TEB) limefanyiwa majaribio nchini China.

Basi hilo linaloendeshwa kwa umeme linauwezo wa kubeba zaidi ya watu 300 .

Basi hilo kubwa lina urefu wa mita 21 na upana wa futi 25 .

Hii ndio mara ya kwanza kwa wabunifu kuonesha basi hilo hadharani baada ya video yake kuvuja katika mitandao mwezi Mei.


Majaribio ya basi hilo la kipekee yalifanyiwa katika barabara iliyofanyiwa ukarabati yenye urefu wa mita 300m.

Basi hilo linauwezo wa kuhudumu kwa kasi ya Kilomita 60 kwa kila saa.

Takriban mabasi hayo manne yanawezwa kuunganishwa na hivyo kuwa na dereva mmoja.

''Mabasi haya ni ya kipekee na moja ya faida yake kuu ni uwezo wake wa kubeba abiria wengi sana 300 kwa kila basi, pia itaokoa sana nafasi barabarani'' alisema mhandisi mkuu katika mradi huo mpya wa usafiri Song Youzhou.

''Inahudumu kama vile treni za kisasa za umeme ila gharama ya kuwekeza kujenga njia na ukarabati barabarani ikiwemo ujenzi wa vituo maalum vya TEB ni 1/5 '.BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: