BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS MAGUFULI AMTEUA LUTENI JENERALI MABEYO KUWA MKUU WA MAJESHI YA ULINZI TANZANIA

 
Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange.
 
Rais John Pombe Magufuli amemteua Luteni Jenerali Venance Mabeyo kuwa mkuu wa majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania akichukua mahala pake jenerali Davis Mwamunyange aliyestaafu.

Taarifa kutoka ikulu iliotumwa katika vyombo vya habari inasema kuwa Luteni huyo sasa amepandishwa cheo na kuwa jenerali kamili.
Mkuu mpya wa majeshi nchini Tanzania Jenerali Venance Mabeyo

Magufuli: Sijazima demokrasia Tanzania
Wakati huohuo rais amemteua meja jenerali James Mwakibolwa kuwa mnadhimu mkuu wa majeshi ya ulinzi akichukua mahala pake Jenerali Mabeyo.Pia yeye alipandishwa cheo cha luteni jenerali.

Rais amesema kuwa uteuzi huo unaanza kutekelezwa mara moja.Tarehe ya kuapishwa kwa wawili hao itatangazwa baadaye
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: