BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP AWA TISHO ULAYA, VIONGOZI WAHAHA


Rais wa Baraza la muungano wa Ulaya Donald Tusk ameonya kwamba maamuzi ya kutia wasiwasi yanayofanywa na Donad Trump ni miongoni mwa chanagmoto zinazokumba muungano huo.

Amesema kuwa mabadiliko yaliofanyika nchini Marekani ni miongoni mwa vitisho kutoka nje vinavyojumuisha China, Urusi na Waislamu wenye itikadi kali kwa muungano huo.

Katika barua kwa viongozi 27 wa bara Ulaya bw Tusk pia amesema kuwa anaamini kwamba wote wanakubaliana naye.

Taarifa kadhaa kutoka Washington zimesababisha maandamano dhidi ya Trump katika miji mikuu ya Ulaya.

Katika barua iliotolewa kabla ya kikao cha muungano huo huko Malta wiki hii, Bw Tusk alisema kuwa utawala mpya wa Donald Trump umeiweka EU katika hali ngumu kwa kuwa unahoji sera ya kigeni ya Marekani ya miaka 70 iliopita.

Alimalizia kwa kusema: Hatuwezi kusalimu amri kwa wale wanaotaka kudhoofisha ushirikiano wetu ambao bila amani hauwezi kufanikiwa.

Tunawakumbusha marafiki zetu wa Marekani kwamba Umoja ndio nguvu.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: