MKUU WA MKOA AMKABIDHI MAKAMU WA RAIS TAARIFA YA UTATUZI WA MIGOGORO YA ARDHI NA UREJESHAJI EKOLOJIA MTO RUAHA MKUU
Makamu Wa Rais, Samia Hassan Suluhu amepongeza kazi nzuri iliyofanya na uongozi wa Mkoa wa Mbeya na timu ya watalaam huku akihaidi kuifanyia kazi ili kufikia malengo ya kumaliza migogoro ya ardhi na urejeshaji ekolojia ya Mto Ruaha.
Licha ya kupongeza Makamu wa rais, Samia Suluhu amekabidhiwa taarifa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla yenye mapendekezo ya namna ya kumaliza migogoro ya vijiji 33 na hifadhi ya Ruaha ili kurejesha ekolojia ya Mto Ruaha Mkuu leo.
Samia pia amefanya mazungumzo na mkuu huyo wa mkoa ofisini kwake wakati wa ziara yake.
0 comments:
Post a Comment