BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KIUNGO WA KLABU YA SIMBA SC JAMES KOTEI HAJUI BINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA, ASUBIRI POINTI ZA KAGERA SUGAR KUTOKA FIFA

Msikie alichosema kiungo wa Simba, Mghana James Kotei eti mpaka sasa alikuwa hajui bingwa wa Ligi Kuu Bara ni nani.

Tangu siku ile Simba walipogomea medali ya mshindi wa pili kwa madai ya kutaka warudishiwe pointi tatu za mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar na kwamba wamepeleka malalamiko Fifa, Mghana Kotei yeye bado anasikilizia.

Kotei anaamini ule mpango bado upo na hataki kusikia kwamba Yanga ndiyo mabingwa.

"Hivi bingwa wa Ligi Kuu ni nani mpaka sasa ni Yanga au Simba," aliuliza Mghana. "Nakumbuka kulikuwa na utata wa zile pointi zetu ilikwenda vipi, alisema Kotei aliyeongezwa mkataba mpya alipowasili nchini baada ya ule wa kwanza wa miezi sita kumalizika.Mwananchi
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: