BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NCHI YA URUSI YATAKA SUDANI KUSINI ICHUNGUZWE.

Mwanajeshi wa Sudan Kusini
URUSI imetoa wito kwa Sudan Kusini iwape adhabu wale waliohusika na kudungua helikopta ya Umoja wa Mataifa hapo Ijumaa na kuwauwa Warusi wane waliokuwamo humo.

Wizara ya Mashauri ya Nchi za Nje ya Urusi ilisema kuwa uchunguzi unafaaa kufanywa sawasawa.

Umoja wa Mataifa ulisema kuwa helikopta hiyo ilidunguliwa na jeshi la Sudan Kusini katika jimbo la Jonglei.

Waziri wa Habari wa Sudan Kusini, Barnaba Marial Benjamin, alisema hapo jana kwamba sababu ya tukio hilo haijulikani na kwamba helikopta hiyo ilikuwa ikiruka katika eneo lenye wapiganaji.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: