BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIA 39 WAUWAWA NCHINI KENYA, KABILA LA POKOLO LATUMIA SILAHA ZA ASILI KUFANYA MAUAJI NA KUCHOMA NYUMBA MOTO 45.

  Wanavijiji wakiangalia maiti kufuatia mapambano ya kikabila huko Kipao, Tana River, Kenya, Dec. 21, 2012.
Wanavijiji wakiangalia maiti kufuatia mapambano ya kikabila huko Kipao.

MAAFISA wa serikali nchini Kenya wanasema watu wasiopungua 39, wanavijiji 30 na washambuliaji tisa wameuwawa katika mapambano mengine  mapya kati ya makundi mawili hasimu ya kikabila katika mkoa wa kusini mashariki wa Tana River.

Ofisa mmoja wa polisi katika eneo anasema kundi la kabila la Pokomo lililokuwa limebeba mishale na bunduki  lilivamia kijiji cha watu wa Orma, alfajiri ya Ijumaa.
http://gdb.voanews.eu/D6FAEBF9-6F53-4926-96C1-4956379E4EB8_w443_r1.jpg

Shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya linasema watoto 13 na wanawake sita walikuwa miongoni mwa waliouwawa katika shambulizi kwenye kijiji cha Kipao. Inasema kiasi cha nyumba 45 zilichomwa moto.

Polisi wanasema wanafahamu  mahali washambuliaji wanakotoka na wanawafuatilia.


Makundi hayo mawili yamefanya mifululizo ya mashambulizi ya mauaji na mashambulizi mengine kama sehemu ya mgogoro unaoendelea juu ya ardhi na maji.

Mwezi wa Agosti na Septemba zaidi ya watu 100 waliuwawa katika mapambano kati ya kabila la Pokomo ambayo ni jamii kubwa ya wakulima na kabila la Orma ambalo linafahamika kwa ufugaji.


Umoja wa Mataifa unasema baadhi ya mauaji huenda yanahusiana na kuongezeka kwa mivutano  kuhusu  uchaguzi mkuu mwaka ujao.


Zaidi ya watu 1,100 waliuwawa katika ghasia za uchaguzi mkuu uliopita nchini Kenya wa mwaka 2007. 

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: