BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SH2.7 MILIONI KUWANG'OA WAFANYABIAHSRA UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM

 JUMLA ya Sh bilioni 2.7, zimetengwa na Serikali, kwa ajili ya kuwalipa fidia wafanyabiashara 120 wa kituo cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo. 

Akizungumza na wadau wa biashara jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi, alisema hadi sasa zaidi ya wafanyabiashara 100 wamelipwa Sh bilioni 2.2, kwa ajili ya kupisha mradi wa mabasi yaendayo kasi.

Alisema lengo la kuwaondoa wafanyabiashara hao, ni kupisha mradi wa mabasi yaendayo kasi, ambayo yanalenga kumaliza tatizo sugu la foleni.

Alisema mradi huo wa Dart, ulitakiwa kukamilika mwaka jana, lakini ulishindikana kutokana na ulipaji wa fidia kwa wafanyabiashara waliopo katika kituo hicho kushindikana.

“Tatizo kubwa la kushindwa kukamilika kwa mradi huu, ni kituo cha mabasi hadi leo (jana), mkandarasi hajaanza kazi, ipo haja kwa wafanyabiashara kukubali hasara ili kufanikisha mradi huo uendelee.

“Mradi huu, utajengwa na mkandarasi kutoka kampuni ya Beijing Constraction, kwa msaada wa Benki ya Dunia ambao unatakiwa kukamilika mwaka 2014/15, kama utashindwa kukamilika mradi utasogezwa mbele au kufutwa kabisa.

“Ni jambo la aibu kwa nchi yetu ya Tanzania, kushindwa kukamilisha mradi huu, kwani katika nchi za wenzetu tayari umeshakamilika mradi huu wa Dart,” alisema Masaburi.

Alisema kutokana na kuchelewa, ipo haja kwa wafanyabiashara hao kuhama kwa hiari yao kabla ya Desemba 30, mwaka huu ili kupisha shughuli kwa mkandarasi kuanza kufanya kazi yake.

Alisema iwapo watashindwa kuhama mpaka Januari mosi, 2013 watatumia nguvu ya Serikali kuvunja maeneo yote.

Alisema mradi wa mabasi yaendayo kasi, yana faida kubwa kwa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam, kwani jumla ya vijana 3,000 watapatiwa mafunzo na wengine kupata ajira.

Alisema jumla ya mabasi 700 ya daladala yataondoshwa kwa ajili ya kuepuka msongamano na kupisha mradi huo ambao utaleta heshima kubwa katika Jiji la Dar es Salaam .

Aliwataka wamiliki wa daladala, kuachana na mabasi hayo na badala yake waanze kununua mabasi makubwa.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: