BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

BALAA IJUMAA KUU: WATU WAWILI WAFARIKI DUNIA NA KUPOTEZA MAISHA BAADA YA GHOROFA KUANGUKA.

JIJI la Dar es Salaam limegubikwa na simanzi nzito kufuatia kuanguka kwa jengo la ghorofa 16 lililopo Mtaa wa Indira Ghandi leo asubuhi.

Ajali hii mbaya imesababisha vifo vya watu 2 na kuacha idadi isiyofahamika, wakiwemo wajenzi na wapita njia, wakiwa wamekwama ndani ya kifusi.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova amewaambia waandishi wetu kuwa waokoaji wamefanikiwa kunusuru watu 15 wakiwa hai.

Taarifa zilizotufikia zinaongeza kuwa magari matatu yameteketea baada ya kuangukiwa na masalia ya jengo hilo, lililokuwa likijengwa na kampuni ya Lucky Construction Limited.

Katika harakati za kuhamasisha shughuli za uokoaji, Rais Jakaya Kikwete, Mwananchi imeelezwa, amewasili katika eneo la tukio.

Hata hivyo, kuna taarifa kuwa shughuli za uokoaji zinakwamishwa na vifaa duni, pamoja na jitihada za ziada kutoka kwa maofisa wa jiji wakishirikiana na Jeshi la Kujenga Taifa na kampuni binafsi ya ulinzi ya Ultimate Security.

Tutawaletea taarifa zaidi kadiri zinavyotufikia
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: