BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAILA ODINGA AWASILISHA KESI MAHAKAMU KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI KUU URAIS KENYA.

MATUKIO YA KISIASA NCHINI KENYA. 
WAANGALIZI WA KIMATAIFA WALISEMA UCHAGUZI WA KENYA ULIKUWA WA AMANI NA MATOKEO YAKE YANAAMINIKA.
President-elect Uhuru Kenyatta displays the certificate from Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) declaring him the winner of the country's presidential election in Nairobi, Mar. 9, 2013. Rais mpya wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Waziri mkuu anayeondoka Raila Odinga akiwahutubia wafuasi wake Nairobi, Machi 16, 2013. Waziri mkuu anayeondoka Raila Odinga akiwahutubia wafuasi wake Nairobi, Machi 16, 2013. 

MGOMBEA urais aliyeshindwa nchini Kenya Raila Odinga, amewasilisha  kesi  katika mahakama kuu jijini Nairobi  Jumamosi kupinga matokeo ya kiti hicho yaliyotangazwa wiki jana.
Mapema Jumamosi  polisi walitumia gesi ya kutoa machozi kutawanya waandamanaji waliokusanyika nje ya mahakama kuu ya Kenya, kuunga  mkono waziri mkuu anayeondoka  Raila Odinga.

Muungano wa chama chake -CORD unasema una imani Bw. Odinga atashinda kesi hiyo. Bw. Odinga alikataa kukubali matokeo ya uchaguzi huo akidai kulikuwa na kasoro wakati wa kuhesabu kura.

Hapo awali Odinga alikuwa ameahidi kama wagombea urais wenzake ,kuwa ataheshimu matokeo ya kiti cha urais.
http://gdb.voanews.com/86AB602E-D160-4746-84FD-3F543D419526_mw384_mh216_s.jpg
Tume huru  ya uchaguzi Kenya, ilimtangaza Bw. Uhuru Kenyatta kuwa mshindi wa urais kwa kuzoa asili mia 50.07 ya kura na hivyo kuepuka uchaguzi wa marudio. 

Waangalizi wa kimataifa na wale wa ndani ya nchi walisema uchaguzi huo ulifanyika kwa njia ya amani na kwamba matokeo yake yanaaminika. 
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: