DC RWEYEMAMU |
Ajali
hiyo imehusisha gari la Halmashauri ya wilaya ya Handeni ambapo watu
wawili wamefariki akiwemo mwandishi wa Habari Hamis Bwanga na Afisa
uhamiaji wa wilaya.
Watu
wanne wamejeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 4.30 leo
asubuhi katika kijiji cha Misima kweye barabara ya Handeni Korogwe
wakiwa kwenye msafara wa kikazi kwenda vijijini kwaajili ya shughuli za
upandaji wa miti kiwilaya.
Mkuu wa
wilaya ya Handeni Muhingo Rweyemamu amesema msafara huo ulikuwa na
magari matatu ikiwemo ya kwake ambayo haijapata ajali.
Amesema
gari hiyo ya halmashauri imepinduka baada ya kuacha njia na kwenda kama
mita mia ambapo iliparamia jiwe na imeharibika vibaya. Kwa mujibu wa
maelezo yake taarifa zaidi zitapatikana baadae kwani kwa sasa
kinachofanyika ni kuwahudumia majeruhi ambao wanakimbizwa katika
hospitali ya rufaa ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro na pia kushughulikia
miili ya marehemu.
Habari hii kwa hisani ya Vedasto Mwamsungu.
0 comments:
Post a Comment