BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

TASWIRA YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UPANDAJI MITI KITAIFA KANDO YA BWAWA LA MINDU MOROGORO.



 Akiandaa kupanda mti.
 Akipanda mti.
 Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii, Maimuna Tarishi akiwa katika matukio matatu tofauti wakati wa maadhimisho ya siku ya upandaji miti kitaifa iliyofanyika kando ya Bwawa la Mindu kata ya Magadu Manispaa ya Morogoro ambapo jumla ya miti 2300 ilipandwa katika eneo hilo mkoani Morogoro.
PICHA JUMAMTANDA.BLOGSPOT.COM
 Makamu Mkuu wa chuo cha kilimo cha Sokoine Morogoro Profesa Gerald Monella naye akipanda mti wakati wa maadhimisho hayo.
 Juma Mtanda, Meneja Blog akipanda mti katika maadhimisho hayo.
 Mhifadhi wa misitu katika safu ya milima ya Uluguru, Sosteness Rwamungira naye akipanda mti.
 Mwanafunzi wa chuo hicho akipanda mti.
 Mfanyakazi wa chuo cha Sokoine Haroun Mpinga akishirki kupanda mti katika maadhimisho hayo.
Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii, Maimuna Tarishiakihutubia wananchi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya upandaji miti kitaifa iliyofanyika Morogoro April 3 mwaka huu.
 Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii, Maimuna Tarishi akiteta jambo na Makamu wa mkuu wa chuo cha kilimo cha Sokoine (SUA) Profesa Gerald Monella.
 Sehemu ya maprofesa wa chuo cha kilimo cha Sokoine Morogoro (SUA) wakifuatilia matukio mbalimbali katika maadhimisho hayo.

Na Juma Mtanda, Morogoro.
SERIKALI imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kusimamia na kuhifadhi misitu ili iweze kuchangia kikamilifu katika kuhifadhi mazingira kwa kutoa mazao na huduma endelevu kukidhi mahitaji ya watanzania wote hususani katika kujiongezea kipato na kuondoa umasikini.

Hayo yalisemwa jana na Katibu mkuu wa Wizara ya maliasili na utalii Maimuna Tarishi kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo Balozi Khamis Kgasheki wakati wa maadhimisho ya siku ya taifa ya kupanda miti iliyofanyika kandokando ya bwawa la Mindu lililopo katika kata ya Magadu Manispaa ya Morogoro.

Katibu Mkuu huyo alisema kuwa baadhi ya hatua zilizochukuliwa na serikali katika kuhifadhi misitu na kutunza mazingira ni pamoja na kuanzishwa na kwa wakala wa huduma za misitu kwa madhumuni ya kuongeza ufanisi na tija katika kusimamia na kuhifadhi rasilimali za misitu na nyuki nchini.

Alisema kuwa takwimu za hivi karibuni zinaonesha kuwa miti inayotumika nchini ni meta za ujazo milioni 87 kwa mwaka na kwamba matumizi hayo ni makubwa ukilinganisha na ukuaji wa miti ambao ni meta za ujazo milioni 76 kwa mwaka.

Aidha alisema kuwa tafiti zilizofanywa sehemu mbalimbali duniani zinaonesha kuwa misitu inatoweka kwa kasi ya nusu kilometa ya mraba kila dakika sika na kwamba iwapo mwenendo huo utaendelea ifikapo mwaka 2035 misitu minene yote duniani ikiwa nia pamoja nay a Tanzania itakuwa imekwisha.

Naye makamu mkuu wa chuo cha Sokoine Sua Profesa Gerald Monella alisema kuwa shughuli za upandaji miti katika chuo hicho zimekuwa zikifanywa kila mwaka na ni moja ya sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya chuo hicho.

Profesa Monella alisema kuwa shughuli za upandaji miti chuoni hapo unalenga katika kuhifadhi ardhi na mazingira, kutunza mipaka ya chuo na shughuli za kitaaluma ambapo katika kipindi hiki cha mwaka 2013-2014 chuo hicho kimepanga kupanda miti 2300 ya mikenge katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye bwawa la mindu.

Shughuli za upandaji miti chuoni hapo kila mwaka zimekuwa zikihudhuliwa na viongozi mbalimbali.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: