BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NCHI YA TANZANIA HATARI KUKUMBWA NA MVUA ZA EL-NINO


Nchi za Afrika Mashariki na kati ikiwamo Tanzania zipo katika wasiwasi wa kukumbwa na mvua za El-nino kutokana na kuongezeka kwa joto katika Bahari ya Pacific.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dk. Agness Kijazi.
 
Akizungumza kwenye mkutano wa 41 wa masuala ya hali ya hewa na utabiri unaofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dk. Agness Kijazi (pichani), alisema kitaalam kuna uwezekano wa kutokea kwa mvua kubwa katika nchi za Afrika Mashariki katika kipindi cha Septemba mpaka Desemba, mwaka huu.

Alisema mkutano huo unawahusisha wataalam mbalimbali kutoka katika nchi 11 na unaangalia mifumo ya hali ya hewa kwa Afrika Mashariki na tayari wameona viashiria vya kutokea kwa mvua hizo.

“Mvua hizo hutokea pale kiwango cha joto kinapoongezeka kwa kiasi kikubwa kwenye bahari na mpaka sasa tumeona joto limeongezeka kwa kiasi kikubwa katika bahari ya Pacific,” alisema Kijazi. 


Alisema baada ya kuangalia mifumo ya hali ya hewa katika eneo la Afrika Mashariki, wataalamu watarudi katika nchi zao na kuangalia mifumo ya hali ya hewa katika maeneo yao na kutoa utabiri kwa wananchi husika kwa kipindi Septemba mpaka Desemba.
 
“Hapa kwetu Tanzania tutatoa utabiri wa mvua kwa miezi mitatu yaani Septemba mpaka Desemaba ifikapo Septemba Mosi mwaka huu,” aliongezea kusema.

Kijazi alitoa wito kwa wananchi na wadau wa hali ya hewa kufuatilia utabiri utakaotolewa Septemba Mosi, mwaka huu ili kujua hali itakavyokuwa. CHANZO: NIPASHE
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: