BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

VIPODOZI VINANE HATARI ZAIDI KWA WANAWAKE WENYE MIMBA



Mbeya. Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, jana ilivitaja vipodozi hatarishi kutumiwa na wajawazito.

Ilisema vipodozi hivyo vilishapigwa marufuku kuingizwa nchini, lakini vinauzwa kinyemela na wafanyabiashara wasio waaminifu.

Kaimu Meneja wa TFDA Nyanda za Juu Kusini, Rodney Alananga, alivitaja vipodozi hivyo kuwa ni
Madhara.

Carolite, Betason, Boss Lotion, Extra Clair, Skin balance Lemon, Top lemon, Lovely body na sabuni ya Jaribu.

Alisema vikitumiwa na wajawazito licha ya kuwaathiri wao, pia huweza kusababisha mtoto aliyeko tumboni akapatwa na mtindio wa ubongo.
Alananga alitoa wito kwa wananchi kuachana na matumizi ya vipodozi hivyo ili kulinda afya zao.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: