Mtoto mmoja kutoka jamii masikini nchini Kenya amesafirishwa hadi shule mpya ya upili anayojiunga nayo kwa helikopta baada ya muungano mmoja wa wanajeshi wa zamani wa angani kusema kuwa utamlipia karo ya shule.
Kelvin Muriuki alikuwa bora katika shule yake katika mtihani wa mwisho wa shule za msingi , lakini umasikini ukamlazimu kufanya kazi katika timbo, familia yake imesema.
Sasa ndoto ya Kelvin imefufuka na anataka kuwa rubani.
Watoto wengi huwacha shule nchini Kenya kutokana na ufukara.
Muungano huo umesema kuwa utamlipia karo Kelvin za dola 530 kila mwaka hadi atakapomaliza shule ya upili 2020.
0 comments:
Post a Comment