BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JESHI LA KENYA KIKOSI CHA WANAMAJI CHAANZA KAZI YA KUSHAMBULIA SOMALIA KATIKA HARATI ZA KUPAMBANA KATIKA NGOME YA MWISHO KWA WANAMGAMBO WA AL-SHABAB MJI WA KISMAYU




JESHI la wanamaji la Kenya limevurumisha mizinga kadhaa katika mji wa bandari wa Kismayu nchini Somalia.

Msemaji wa jeshi hilo, Cyrus Oguna alisema mashambulizi hayo pia yamelenga uwanja wa ndege wa Kismayu. 

Oguna alisema hatua hiyo ni mwanzo wa kuanza mashambulizi kamili ya kikosi cha AU kwa lengo la kuukomboa mji huo kutoka mikononi mwa wanamgambo wa Al-shabab.


Habari zinasema kuwa wanamgambo hao wamejiweka tayari na kuongeza idadi ya wapiganaji wake ili kukabiliana na vikosi vya AMISOM.

Kwa sasa Kismayu ndio mji wa pekee muhimu unaodhibitiwa na wanamgambo hao. 

Bandari ya Kismayu ni moja ya vitega-uchumi muhimu kwa wanamgambo hao na iwapo utatwaliwa na AMISOM itakuwa pigo kubwa kwa Al-shabab wanaotaka kuipindua serikali ya Somalia.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: