BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAGAIDI 14 NCHINI MISRI WAHUKUMIWA KIFO NA MAHAKAMA.

MAHAKAMA nchini Misri imewahukumu kifo magaidi 14 na wengine wanne kifungo cha maisha jela kwa kosa la kushambulia jeshi na maafisa wa polisi katika rasi ya Sinai.

Watu hao ni wafuasi wa kundi moja la wanamgambo ambao wamepatikana na hatia ya kuwaua maafisa watatu wa polisi, mwanajeshi mmoja na raia katika mashambulizi yaliyofanywa mwezi Juni na Julai mwaka 2011.

Eneo la Sinai la Misri kwa muda mrefu limekuwa likikabiliwa na matatizo ya kiuslama. 

Mwezi Agosti mwaka huu jeshi la Misri lilianzisha operesheni kali ya kuimarisha usalama kwenye eneo hilo baada ya watu wasiojulikana kuuwa askari 16 wa mpakani wa Misri.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: