BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAPIGANO YAREJEA TENA DARFUL

 http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2012/10/03/121003172257_unamid_forces_304x171_bbc_nocredit.jpg
WAKUU wa Sudan wanasema watu kadha wamekufa kwenye shambulio lilofanywa na wapiganaji dhidi ya wanajeshi wa serikali katika eneo la Darfur, magharibi mwa nchi.

Afisa mmoja wa serikali alisema wanamgambo wanaounga mkono serikali wameuliwa katika shambulio hilo la ghafla, karibu na al-Fasher, mji mkuu wa jimbo la North Darfur.

Umoja wa wapiganaji - Sudanese Revolutionary Front - ulisema ulifanya shambulio hilo na kuuwa wanajeshi wa serikali na kuteka magari ya jeshi na silaha.

Baadhi ya makundi ya wapiganaji ya Darfur mwaka jana yalitia saini mkataba wa amani na serikali ya Sudan, lakini makundi mengine yanaendelea kupigana.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: