BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JK:IRAN INA NAFASI MUHIMU KIMATAIFA.

Rais Kikwete: Iran ina nafasi muhimu kimataifa 
RAIS Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, nchi yake na Iran zina historia kongwe ya mahusiano. 

Kikwete amesema hayo katika hafla fupi ya kupokea hati ya utambulisho ya balozi mpya wa Iran nchini Tanzania na kueleza kuridhishwa kwake na mwenendo wa kukua uhusiano baina ya Tehran na Dar es Salaam. 

Rais wa Tanzania amesema kuwa, Iran ina nafasi muhimu mno kieneo na kimataifa na kwamba, imepiga hatua kubwa katika nyuga mbalimbali hususan za kielimu na kiteknolojia na kuongeza kuwa, ana matumaini nchi yake itaweza kustafidi na uzoefu wa Iran katika nyanja mbalimbali. 

Rais Kikwete amesema, Tanzania iko tayari kustawisha zaidi uhusiano na Iran. 

Kwa upande wake Mahdi Agha Jaafari, balozi mpya wa Iran nchini Tanzania amesema Iran imeazimia kwa dhati kabisa kukuza ushirikiano wake na Tanzania katika sekta mbalimbali.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: