BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAKAHABA DAR ES SALAAM KUUNDA UMOJA.

MWAKA 2013 umeshuhudia kutokea matukio mbalimbali ya kusikitisha na kusimumua lakini kabla mwaka huu haujaisha kumeibuka kioja baada ya wanawake wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili (makahaba) jijini Dar kuweka dhamila ya kuunda umoja wao na kutoa bei elekezi ya kutoa huduma yao.

Uchunguzi wa waandishi wetu kupitia Oparesheni Fichua Maovu (OFM) chini ya Global Publis

hers umebaini kuwa umoja huo unaitwa UMADA (Umoja wa Makahaba Dar).

Katika makubaliano yao, kuna mambo ya kushangaza ikiwa ni pamoja na kujipangia bei ya pamoja na kupanda kwa kasi ya ajabu kwa bei ya huduma inayotolewa na wanawake hao sehemu mbalimbali jijini Dar huku watakaobainiku kufanya biashara hiyo haramu kwa kujiuza bei chee watakiona cha mtema kuni.


Maeneo ambayo yalifikiwa na OFM na kupewa utaratibu wa huduma ni kama ifuatavyo;
Maeneo ya Jolly Club, Upanga, Dar ilibainika kuwa huduma ya haraka haraka (fastafasta) itakuwa kiasi cha tozo ya Sh. 30,000 na kulala usiku kucha kiasu cha Sh. 100,000.


Maeneo ya Afrika Sana, Sinza, Club Sun Cirro, Ubungo na Club Meridian, Kinondoni, huduma hiyo ya haraka haraka itaghalimu kiasi cha Sh. 10,000 na kulala ni 40,000.


Maeneo ya New Maisha Club, Masaki ni kati ya dola 50 (Sh. 80,000) kwa fastafasta na dola 100 (Sh. 160,000) kulala kwa Mzungu na kwa Mswahili ni Sh. 50,000 kwa huduma ya haraka na Sh. 100,000 kulala.


Maeneo ya Meeda Club, Sinza kuna huduma ya fastafasta tu ambayo hutolewa kati ya Sh. 5,000 had 10,000 huku huduma ya kulala ikifutwa kwenye bajeti ya mwaka huu kwani eneo hilo wapo wengi hadi wanaovaa kandambili.


Huko Uwanja wa Fisi huduma hupatikana kuanzia Sh. 500 hadi 5,000 huku maeneo ya Buguruni ikianzia Sh. 2,000 hadi 10,000.


Katika massage centers (maduka ya kuchua mwili), ilibainika kuwa bei ni kati ya Sh. 50,000 hadi 100,000 kutegemea na kiwango cha mrembo.


Ilifichuka kuwa kwa wale wa maofisini wanaojishughulisha na biashara hiyo kwenye vituop vya ‘masaji’, bei ni kuanzia Sh. 100,000 kwa siku nzima na ni warembo wa haja.


Huko Temeke, Dar ilibainika kuwa wapo hadi wa Sh. 200 huku wale wa vyuo mbalimbali wakianzia Sh. 5,000 hadi 15,000 ambao wengi hupatikana klabu za starehe usiku hasa ‘boom’ likikatika. 


Kwa wale wa vyuoni ilibumburuka kuwa mwanaume akiwa na gari ana uwezo wa kumchukua yule anayemtaka bila kipingamizi.


Katika mahojiano na timu yetu, baadhi ya wanawake hao walifunguka kuwa wamefikia hatua hiyo ya kupandisha bei maradufu kwa sababu kila kitu kimepanda bei kuanzia mavazi, sabuni, vipodozi na nauli hivyo nao ili kuboresha huduma lazima bei ipande.


Gazeti hili linakemea vikali bishara hiyo haramu na kuviomba vyombo husika kuingilia kati ili kuikomesha.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: