BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAJIJI 14 MAKUBWA NAMNA YALIVYOUKARIBIKA MWAKA 2016 NA KUAGANA NA MWAKA 2015 DUNIANI.



Watu katika miji mbalimbali walijitokeza kuukaribisha Mwaka Mpya wa 2016 kwa njia mbalimbali. Huu hapa ni mkusanyiko wa picha za hali ilivyokuwa.

Australia ilikuwa moja ya nchi za kwanza kuingia mwaka 2016, fataki zinaonekana hapa juu ya jumba la Opera House na daraja la Harbour Bridge.Mjini Sydney

Nchini Misri, fataki zinaonekana zikilipuka karibu na Piramidi.Mjini Cairo.

Jijini Berlin, fataki zilitawala anga kama inavyoonekana hapa juu ya Lango la Brandenburg mjini Berlin.Mjini Berlin

Mjini London, hivi ndivyo hali ilivyokuwa karibu na Big Ben. Maelfu ya watu walijitokeza kutazama fataki.Mjini London

Mji wa Baghdad haukuachwa nyuma, na hapa fataki zinaonekana zikilipuka katika Bustani ya Zawra.Mjini Baghdad

Mjini Singapore, mwaka mpya ulikaribishwa kwa fataki. Hapa ni Marina Bay.Mjini Singapore
Mjini Kuala Lumpur, nchini Malaysia fataki zinaonekana zikilipuka karibu na jengo mashuhuri ya Petronas Towers.Mjini Kuala Lumpur

Mjini Taipeni, Taiwan, fataki zinaonekana kwenye jumba refu la Taipei 101.Mjini Taipei

Mjini Paris, watu walikusanyika Champs Elysees kutazama video ya Mwaka Mpya iliyoonyeshwa katika Arc de Triomphe.Mjini Paris

Nchini India, mwanamume huyo alitumia nyanya, vitunguu na pilipili kuandika 2016.
Mjini Amristar, India

Mjini Auckland, New Zealand fataki zililipuliwa katika jumba la Auckland Sky Tower, mkesha wa Mwaka MpyaFataki New Zealand

Hapa, mwanamume anaonekana akitembea karibu na mapambo yaliyoandika 2016 katika mji wa Kiev, nchini Ukraine. GDP ya taifa hilo ilishuka asilimia 9 mwaka 2015.Mjini Kiev

Mjini Brazil, baadhi waliamua kufika katika ufuko wa Copacabana mjini Rio de Janeiro kuukaribisha mwaka mpya.Mjini Rio

Mjini Beijing watu wengi waikusanyika kwa hafla iliyokuwa Hekalu la Tai Miao karibu na Forbidden City mjini Beijing.Mjini Beijing
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: