BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WABUNGE KUPIGA KURA YA KUMCHAGUA RAIS MPYA UWANJA WA NDEGE SOMALIA

Milipuko imesikika katika mji Mkuu wa Mogadishu nchini Somalia usiku wa kuamkia leo wabunge wanapotarajiwa kukutana kumchagua rais mpya.

Kumekuwa na taarifa kuwa mizinga imelipuliwa karibu na uwanja wa ndege ambapo uchaguzi unatarajiwa kufanyika, huku wakazi wa eneo la Waberi iliyoko Kusini Magharibi mwa Mogadishu pia wakithibitisha kusikia milipuko.

Kufikia sasa hakuna maafa au majeruhi walioripotiwa ingawa hali ya wasiwasi imetanda Mogadishu.

Barabara zote zimefungwa. Uwanja wa ndege hakuendeki. Na hata wakazi wengine hawawezi kuvuka kutoka barabara hii hadi ile.

Mahali pa kufanyia uchaguzi pamehamishwa, kutoka Chuo cha Polisi hadi Uwanja wa ndege wa Mogadishu wenye ulinzi mkali. Sababu ya kuongezeka kwa vitisho vya usalama na rushwa .

Hivi leo ndege hazitaruhusiwa kutua au kupaa kutokea uwanja huu, kwa kuwa ni siku ya kupiga kura. Mji wa Mogadishu

Mfumo wa uchaguzi nchini Somalia umeharibika kama ilivyo miundombinu yake.

Haina daftari la wapiga kura. Wabunge mia tatu na ishirini na tisa ndio watakaomchagua Rais ajaye.

Lakini sasa tuhuma za rushwa zinatishia kuvuruga mchakato mzima. Kuna tuhuma nzito kuwa wabunge wengi wamelipwa mamilioni ya dola kushawishi upiga-kura wao.

Wanawake wengi zaidi watashiriki kupiga kura wakati huu, hivyo kufanya asilimia ishirini na sita ya kura zote za bunge.

Ingawa wanawake wawili waliotangaza nia ya kuwania Urais akiwemo Fatuma Dayyib aliyetangazwa sana, walijitoa.
Licha ya maswali mengi kuhusu uchaguzi huu, wananchi wa Somalia wanatumai kuwa kufanikiwa kwa uchaguzi huu utawaongoza kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020. Lakini kwanza, nchi inahitaji Rais na serikali inayofanya kazi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: