BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

UJAZO WA GUNIA LA MKAA MWISHO KILO 50, UKIZIDI TU UNAPIGWA FAINI YA NGUVU

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umewataka wasafirishaji na wauzaji wa mkaa nchini, kuhakikisha ujazo wa mkaa hauzidi kilo 50 ili kuepuka adhabu inayotokana na kukiuka Sheria ya Vipimo nchini.

Hata hivyo, katika maeneo mbalimbali nchini, bado wauzaji wa bidhaa hiyo wanauza kwa ujazo unaozidi kiwango hicho huku wengine wakiwa hawafahamu kuhusu uwapo wa sheria hiyo.

Akizungumza katika maonyesho ya Wakulima maarufu kwa jina la Nanenane jana, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa TFS, Glory Mziray alisema sheria ya vipimo inataka bidhaa hiyo kupimwa katika ujazo wa kilo 50.

“Tunawataka wauzaji na wasafirishaji kuzingatia sheria hii ili kuepuka adhabu inayotokana na ukiukwaji wa sheria,” alisema Mziray.

Pia, alisema ushuru wa vitanda umepungua kutoka Sh120,000 mwaka uliopita hadi Sh 20,000 mwaka huu, huku ushuru wa mlango ukipungua kutoka Sh90,000 mwaka jana hadi Sh50,000 mwaka huu.

Hata hivyo, alisema watu wanaotaka maelezo zaidi kufika katika ofisi za wakala huo, kuangalia katika tovuti na mitandao ili kukidhi matakwa ya sheria hizo. 


Muuzaji mkaa mkoani hapa, Rashid Maulid alisema ni vigumu kutekeleza sheria hiyo kutokana na wengi kutokuwa na mizani ya kupimia.Mwananchi
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: